64 – Anas ameeleza:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema wakati ambapo jeneza la Sa´d lilikuwa tayari kwa ajili ya kuswaliwa: ”´Arshi ya Mwingi wa rehema imetikisika kwa ajili yake.”[1]
Hii ni Swahiyh.
65 – Abu Sa´iyd amesimulia ya kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”´Arshi ilitikisika kwa ajili ya kifo cha Sa´d bin Mu´aadh.”[2]
Hadiyth hii ni Swahiyh.
66 – Usayd bin Hudhwayr amesimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
”´Arshi ilitikisika juu ya kifo cha Sa´d.”
Cheni yake ya wapokezi ni nzuri.
67 – Rumaythah amesema:
”Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema – na ningelitaka kubusu muhuri wake kwa jinsi nilivyokuwa karibu basi ningelifanya: ”Imetikisika ´Arshi ya Mwingi wa huruma.”
Akimkusudia Sa´d bin Mu´aadh. Cheni hii imesalimika[3]. Ibn Mandah ameisahihisha. Hadiyth hiyohiyo imesimuliwa na Sa´d bin Abiy Waqqaas, Ibn ´Umar, Hudhayfah, Abu Hurayrah, Asmaa’ bint Yaziyd na Mu´ayqiyb. Kwa hiyo yamepokelewa kwa mapokezi tele. Nashuhudia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameyasema.
[1] Muslim na wengineo. Tazama “Dhwilaal-ul-Jannah” (561).
[2] Ahmad na Ibn Sa´d. Tazama “Dhwilaal-ul-Jannah” (564-567).
[3] Hili linahitaji kuangaliwa vyema, kama nilivyobainisha katika “Dhwilaal-ul-Jannah” (567). Katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd” (1/137-138 – muswada) kuna mlango maalum juu ya Hadiyth hii. Humo amekusanya cheni za wapokezi za Hadiyth hiyo.
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk. 109-110
- Imechapishwa: 26/06/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
64 – Anas ameeleza:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema wakati ambapo jeneza la Sa´d lilikuwa tayari kwa ajili ya kuswaliwa: ”´Arshi ya Mwingi wa rehema imetikisika kwa ajili yake.”[1]
Hii ni Swahiyh.
65 – Abu Sa´iyd amesimulia ya kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”´Arshi ilitikisika kwa ajili ya kifo cha Sa´d bin Mu´aadh.”[2]
Hadiyth hii ni Swahiyh.
66 – Usayd bin Hudhwayr amesimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
”´Arshi ilitikisika juu ya kifo cha Sa´d.”
Cheni yake ya wapokezi ni nzuri.
67 – Rumaythah amesema:
”Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema – na ningelitaka kubusu muhuri wake kwa jinsi nilivyokuwa karibu basi ningelifanya: ”Imetikisika ´Arshi ya Mwingi wa huruma.”
Akimkusudia Sa´d bin Mu´aadh. Cheni hii imesalimika[3]. Ibn Mandah ameisahihisha. Hadiyth hiyohiyo imesimuliwa na Sa´d bin Abiy Waqqaas, Ibn ´Umar, Hudhayfah, Abu Hurayrah, Asmaa’ bint Yaziyd na Mu´ayqiyb. Kwa hiyo yamepokelewa kwa mapokezi tele. Nashuhudia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameyasema.
[1] Muslim na wengineo. Tazama “Dhwilaal-ul-Jannah” (561).
[2] Ahmad na Ibn Sa´d. Tazama “Dhwilaal-ul-Jannah” (564-567).
[3] Hili linahitaji kuangaliwa vyema, kama nilivyobainisha katika “Dhwilaal-ul-Jannah” (567). Katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd” (1/137-138 – muswada) kuna mlango maalum juu ya Hadiyth hii. Humo amekusanya cheni za wapokezi za Hadiyth hiyo.
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk. 109-110
Imechapishwa: 26/06/2024
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/67-arshi-imetikisika-wakati-alipokufa/