Swali 332: Ni kipi ukijuacho kuhusu Hadiyth ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah amlaani mwanamke mwenye kunyanyua sauti yake japokuwa ni kwa kumtaja Allaah”?
Jibu: Hadiyth ambayo haikuthibiti. Mola (´Azza wa Jall) amesema katika kitabu Chake kitukufu:
وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا
“Semeni kauli inayokubalika.” (33:32)
فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ
”Msilegeze kauli asije akaingiwa tamaa ambaye moyoni mwake mna maradhi.” (33:32)
Lau mwanamke atasema “Subhnaan Allaah”, “Allaahu Akbar” na akatamja Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) hakuna neno juu yake – Allaah akitaka.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 573
- Imechapishwa: 15/12/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)
Related
Wanafunzi wa kiume kusoma kwenye klasi moja na wanafunzi wa kike na kupeana mikono
Swali: Ni ipi hukumu kwa mwanamke kuwasalimia wanafunzi wenzake darasani kwa kupeana mikono? Ni ipi hukumu endapo yeye mwanamke atanyoosha mkono wake kumsalimia? Jibu: Haijuzu kusoma kwa kuchanganyikana na wasichana sehemu moja au klasi moja. Hii ni katika sababu kubwa za mtihani. Haijuzu kwa wanafunzi wa kiume wala wa kike…
In "Masomo ya mwanamke"
Wanawake kuzipamba sauti zao za Qur-aan mbele ya mwalimu wa kiume
Swali: Dada huyu anauliza ni ipi hukumu ya wanafunzi wa kike kuremba sauti zao wakati wa kusoma Qur-aan mbele ya mwalimu wa kiume katika chuo kikuu pamoja na kuwa mwanamke hakutakiwa kufanya hivo? Jibu: Sionelei apambe sauti yake. Kwa sababu Allaah (Ta´ala) amesema: فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ…
In "Masomo ya mwanamke"
Hapa mwanamke anaweza kutoka nyumbani kwake kwa wingi
Swali: Je, inafaa kwa mwanamke wa Kiislamu kutoka kwa wingi nje ya nyumba kwa ajili ya kulingania kwa Allaah? Jibu: Hiki ni kitendo chema. Mwanamke kutoka kwa ajili ya kulingania ni kitendo chema. Maneno Yake: وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ “Kaeni majumbani mwenu.”[1] Maamrisho ya kutulizana nyumbani ni pale ambapo hakuna haja.…
In "Mwanamke kufanya Da´wah"