56. Vitu vinne Allaah ameviumba kwa mkono Wake

53 – Mujaahid ameeleza kwamba ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

”Allaah ameviumba vitu vinne kwa mkono Wake: ´Arshi, kalamu, Aadam na Pepo ya Edeni. Kisha akaviumba viumbe vyengine: ”Kuweni!” na vikawa.”[1]

Cheni ya wapokezi wake ni nzuri.

[1] ad-Daarimiy, Abush-Shaykh katika “al-´Adhwamah” na al-Laalakaa’iy. Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za Muslim.

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk. 105
  • Imechapishwa: 24/06/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy