Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Halafu mtu anaenda kwenye Rukuu´, kuinuka kutoka kwenye Rukuu´, kunyooka sawasawa, kusujudu juu ya viungo saba na kuinuka kutoka hapo na kukaa baina ya Sajdah mbili. Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ارْكَعُوا وَاسْجُدُوا
“Enyi mloamini! Rukuuni na sujuduni.”[1]
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Nimeamrishwa kujusudu juu ya viungo saba.”[2]
MAELEZO
Maneno yake:
“Nguzo ya nne miongoni mwa nguzo za swalah ni Rukuu´.”
Maana ya Rukuu´ ni kuinama, kuweka mikono yako kwenye magoti yako, kuachanisha vidole vyako na kuutandaza na kuuweka sawa mgongo wako na useme:
سبحان ربي العظيم
“Ametakasika Mola wangu aliyetukuka.”
Ambaye hatosema hivo swalah yake haitosihi.
[1] 22:77
[2] al-Bukhaariy (810) na Muslim (490).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 87
- Imechapishwa: 21/06/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket