Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) amesema:
Hadiyth nyingine inasema:
“Wamegawanyika mayahudi katika mapote sabini na moja, wakagawanyika manaswara katika mapote sabini na mbili na Ummah wangu utagawanyika mapote sabini na tatu – yote hayo yataingia Motoni ila moja tu.” Maswahabah wakauliza: “Ni lipi hilo, ewe Mtume wa Allaah?” Akasema: “Ni lile litalokuwa katika mfano wa yale niliyomo mimi na Maswahabah zangu.”[1]
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna dalili juu ya kupotea na kupinda kwa mayahudi na manaswara. Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ni lile litalokuwa katika mfano wa yale niliyomo mimi na Maswahabah zangu.”
Nao ni Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah, nao ni kundi lililookoka, nao ni kundi lililonusuriwa. Yote haya ni majina yao. Nao ni Maswahabah, Taabi´uun na wale watakaofuata mfumo wao.
Hii ni habari njema. Ni lazima kubaki kundi lililo juu ya haki ambalo linafuata njia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na linalofanya mfano wa matendo ya Maswahabah. Haki na ufuataji hautosita katika Ummah huu.
[1] Ibn Maajah (3992), at-Tirmidhiy (2641) na Abu Daawuud (4596). at-Tirmidhiy amesema:
“Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 86
- Imechapishwa: 21/06/2022
Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) amesema:
Hadiyth nyingine inasema:
“Wamegawanyika mayahudi katika mapote sabini na moja, wakagawanyika manaswara katika mapote sabini na mbili na Ummah wangu utagawanyika mapote sabini na tatu – yote hayo yataingia Motoni ila moja tu.” Maswahabah wakauliza: “Ni lipi hilo, ewe Mtume wa Allaah?” Akasema: “Ni lile litalokuwa katika mfano wa yale niliyomo mimi na Maswahabah zangu.”[1]
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna dalili juu ya kupotea na kupinda kwa mayahudi na manaswara. Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ni lile litalokuwa katika mfano wa yale niliyomo mimi na Maswahabah zangu.”
Nao ni Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah, nao ni kundi lililookoka, nao ni kundi lililonusuriwa. Yote haya ni majina yao. Nao ni Maswahabah, Taabi´uun na wale watakaofuata mfumo wao.
Hii ni habari njema. Ni lazima kubaki kundi lililo juu ya haki ambalo linafuata njia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na linalofanya mfano wa matendo ya Maswahabah. Haki na ufuataji hautosita katika Ummah huu.
[1] Ibn Maajah (3992), at-Tirmidhiy (2641) na Abu Daawuud (4596). at-Tirmidhiy amesema:
“Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 86
Imechapishwa: 21/06/2022
https://firqatunnajia.com/52-habari-njema-kwa-ahl-us-sunnah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)