1 – Ee mwanangu kipenzi! Lazimiana kumcha Allaah na kumtii. Jiepushe na maharamisho Yake kwa kufuata njia Yake na alama za njia ili yarekebike mapungufu yako na uwe mwenye furaha.
2 – Mtii baba yako na tosheka na nasaha zake. Yazingatie hayo kikamilifu.
3 – Nakutahadharisha na porojo na kucheka sana, mizaha na kuwadhihaki ndugu. Kwani hayo yanaondosha heshima na kuleta chuki.
4 – Hakikisha ni mwenye thamani na heshima pasi na kuwa na kiburi wala majivuno.
5 – Mpokee rafiki na adui yako kwa uso wenye maridhawa. Jizuie na kuwadhuru pasi na kuwadhalilisha wala kuwaogopa.
6 – Kuwa mkati na kati katika mambo yako yote. Bora ya mambo ni yale ya kati na kati.
7 – Zungumza machache.
8 – Wasalimie watu.
9 – Tembea kwa kunyooka na kati na kati.
10 – Usikae kwenye masoko wala usifanye maduka yakawa ndio mahali pa makutano yako.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Hibbaan al-Bustiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Rawdhat-ul-´Uqalaa’ wa Nuzhat-ul-Fudhwalaa’, uk. 198
- Imechapishwa: 18/08/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket