44 – Kisha akapokea kutoka kwa Sa´d, ambaye amesimulia kuwa ´Imraan amesema:
”Nilikuwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati kundi la watu kutoka katika Banuu Tamiym lilipomjia. Akasema: ”Zipokeeni khabari njema, ee Banuu Tamiym!” Wakasema: ”Umetubashiria, hivyo tupe basi!” Likaingia kundi la wayemeni. Akasema: ”Zipokeeni khabari njema, enyi watu wa Yemen, kwani Banuu Tamiym hawakuzikubali.” Wakasema: ”Tumezipokea. Tumekujia ili tupate kuielewa dini na kukuuliza juu ya mwanzo wa jambo hili.” Akasema: ”Allaah alikuwepo na hakukuwa chochote kabla Yake. ´Arshi Yake ilikuwa juu ya maji. Akaziumba mbingu na ardhi na akaandika kwenye Ukumbusho kila kitu.” Halafu akanijia bwana mmoja na kusema: ”Ee ´Imraan! Kamshike ngamia wako ameenda.” Nikaondoka kumtafuta na nikamuona yuko mbali. Naapa kwa Allaah natamani endapo angekimbia na nisingesimama.”[1]
Napata uzito pindi ninapotaja dalili zote hizi kwa lengo la kusimamisha hoja. Hujamsikia mshairi akisema:
Hakuna kitu kinachokuwa sawa katika akili
ikiwa mwanga wa mchana unahitaji kufahamishwa?
[1] al-Bukhaariy (7418).
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 102
- Imechapishwa: 24/06/2024
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
44 – Kisha akapokea kutoka kwa Sa´d, ambaye amesimulia kuwa ´Imraan amesema:
”Nilikuwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati kundi la watu kutoka katika Banuu Tamiym lilipomjia. Akasema: ”Zipokeeni khabari njema, ee Banuu Tamiym!” Wakasema: ”Umetubashiria, hivyo tupe basi!” Likaingia kundi la wayemeni. Akasema: ”Zipokeeni khabari njema, enyi watu wa Yemen, kwani Banuu Tamiym hawakuzikubali.” Wakasema: ”Tumezipokea. Tumekujia ili tupate kuielewa dini na kukuuliza juu ya mwanzo wa jambo hili.” Akasema: ”Allaah alikuwepo na hakukuwa chochote kabla Yake. ´Arshi Yake ilikuwa juu ya maji. Akaziumba mbingu na ardhi na akaandika kwenye Ukumbusho kila kitu.” Halafu akanijia bwana mmoja na kusema: ”Ee ´Imraan! Kamshike ngamia wako ameenda.” Nikaondoka kumtafuta na nikamuona yuko mbali. Naapa kwa Allaah natamani endapo angekimbia na nisingesimama.”[1]
Napata uzito pindi ninapotaja dalili zote hizi kwa lengo la kusimamisha hoja. Hujamsikia mshairi akisema:
Hakuna kitu kinachokuwa sawa katika akili
ikiwa mwanga wa mchana unahitaji kufahamishwa?
[1] al-Bukhaariy (7418).
Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 102
Imechapishwa: 24/06/2024
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/47-allaah-alikuwepo-na-hakukuwepo-kitu-kabla-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)