199 – Kaamil bin Twalhah ametukhabarisha: Mubaarak ametukhabarisha, kutoka kwa al-Hasan, kutoka kwa Anas, ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alimwambia ´Umar: “Je, huridhii wao kuwa na dunia na sisi Aakhirah?”[1]
200 – Ibn Kaasib ametukhabarisha: Sufyaan bin ´Uyaynah ametukhabarisha, kutoka kwa Yahyaa bin Sa´iyd na ´Amr bin Diynaar, kutoka kwa Ma´mar, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa Hind, kutoka kwa Umm Salamah, ambaye ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Pengine ambaye amevaa duniani akawa uchi siku ya Qiyaamah.”[2]
201 – ´Amr bin Shu´ayb ametukhabarisha: Bishr bin Shu´ayb ametukhabarisha, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa Hind, kutoka kwa Umm Salamah, ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Pengine ambaye amevaa duniani akawa uchi siku ya Qiyaamah.”
[1] Ahmad (12009). Swahiyh kwa mujibu wa al-Mundhiriy katika “at-Targhiyb wat-Tarhiyb” (4/175).
[2] al-Bukhaariy (5844).
- Muhusika: Imaam Abu Bakr Ahmad bin Abiy ´Aaswim ash-Shaybaaniy (a.f.k. 287)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-uz-Zuhd, uk. 51-52
- Imechapishwa: 14/07/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
Related
24. Dunia ni tamu na ya kijani kibichi
149 – Husayn bin Hasan bin Harb ametukhabarisha: ´Abdullaah bin al-Mubaarak ametukhabarisha, kutoka kwa Yuunus, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa ´Urwah na Sa´iyd bin al-Musayyab, ambao wameeleza kuwa Hakiym bin Hizaam ambaye: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) aliniambia: “Ee Hakim! Hakika dunia ni tamu na ya kijani…
In "Kitaab-uz-Zuhd – Ibn Abiy ´Aaswim"
43. Pindi wapumbavu watapoishika dunia
192 – Hishaam bin Khaalid ametukhabarisha: al-Waliyd bin Muslim ametukhabarisha, kutoka kwa Ibn Lahiy´ah, kutoka kwa ´Uqayl, kutoka kwa az-Zuhriy: ´Abdul-Malik bin Abiy Bakr bin ´Abdir-Rahmaan, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Dharr, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: "Qiyaamah hakitosimama mpaka mpumbavu,…
In "Kitaab-uz-Zuhd – Ibn Abiy ´Aaswim"
19. Kumuua muumini ni jambo kubwa zaidi
137 – Abu Salamah Yahyaa bin Khalaf ametukhabarisha: Ibn Abiy ´Adiy ametukhabarisha, kutoka kwa Shu´bah, kutoka kwa Ya´laa bin ´Atwaa’, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Amr, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambaye amesema: “Kuondoka kwa ulimwengu ni jambo jepesi rahisi zaidi mbele ya Allaah…
In "Kitaab-uz-Zuhd – Ibn Abiy ´Aaswim"