40. Mapendekezo ya kuomba kinga kabla ya kuanza al-Faatihah

Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:

Kisha mtu anasema:

أعوذُ بِٱللَّهِ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

“Najilinda kwa Allaah kutokamana na  Shaytwaan aliyefukuzwa na kuwekwa mbali.”

Maana ya:

أعوذُ بِٱللَّهِ

“Najilinda kwa Allaah… “

bi maana ninaomba kinga na msaada Kwako, ee Allaah.

Maana ya:

مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

“… kutokamana na  Shaytwaan aliyefukuzwa mbali.”

bi maana aliyefukuzwa na kuwekwa mbali na rehema za Allaah, kutokana na kunidhuru duniani na Aakhirah.

MAELEZO

Baada ya du´aa ya kufungua swalah na kabla ya kuanza kusoma aombe kinga kwa Allaah, jambo ambalo limetajwa na Shaykh na kulipambanua. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:

فَإِذَا قَرَأْتَ الْقُرْآنَ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ

“Unapotaka kusoma Qur-aan basi, omba ulinzi kwa Allaah kutokamana na shaytwaan aliyefukuzwa mbali.”[1]

Kwa maana unapotaka kuisoma. Ibn Kathiyr amesema katika tafsiri ya Aayah hii:

“Hii ni amri ya kupendeleza si ya lazima. Abu Ja´far Ibn Jariyr na maimamu wengine wamepokea kauli ya maafikiano kuhusu hilo.”

[1] 16:98

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 46
  • Imechapishwa: 02/06/2026