35. Muuliwaji na muuaji siku ya Qiyaamah

33 – Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Muuliwaji atakuja na muuaji siku ya Qiyaamah. Atakuwa amekishika kichwa chake mkononi mwake na damu ikitoka kwenye mishipa yake, aseme ”Ee Mola wangu! Aliniua!” mpaka asogezwe karibu Naye kwenye ´Arshi.”[1]

[1] Swahiyh. Ahmad na wengineo wameipokea kwa cheni mbili Swahiyh kutoka kwake. Nimeikagua katika “al-Mushkaah” (3465).

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 96-97
  • Imechapishwa: 24/06/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy