Mfano wa soksi hauhitaji kuungwa mkono maana yake ya kilugha na ya Kishari´ah. Inajulikana kwa kila mtu kutokana na nukuu za wanazuoni kuhusu maana yake, kwa sababu hilo ni katika mlango wa kufafanua yaliyo wazi. Lakini kilichotulazimisha kufanya hivyo ni yale tuliyoyaona katika baadhi ya vitabu vya wale waliodai kwamba soksi ni soksi za ngozi zinazovaliwa juu ya soksi za ngozi hadi kwenye vifundo kwa ajili ya baridi na kulinda soksi za ngozi ya chini dhidi ya uchafu na maji ya kuosha. Mwingine akaifungamanisha na kuwa ni ya ngozi. Haya ni makosa katika lugha, desturi na Fiqh pia, kwa sababu kinachodaiwa hapo ni buti na si soksi. Cha kushangaza ni maneno ya al-Jazuuliy miongoni mwa wanazuoni wa Maalikiyyah:
”Wametofautiana kuhusu soksi na vuti na kama ni vitu viwili tofauti au ni kitu kimoja.”
Chanzo cha tofauti hiyo ni yale yaliyopokewa katika ”at-Tawdhwiyh” ya kwamba Imaam Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) alitafsiri buti kuwa ni soksi iliotiwa ngozi chini na juu, basi wakadhania kutokana na hilo kwamba soksi haiwi isipokuwa hivyo tu, ilihali soksi ikiwekewa ngozi kwa sifa hiyo na kuitwa buti, haimaanishi kuwa kila soksi ni buti, kwa sababu soksi hujumuisha yenye ngozi na isiyokuwa na ngozi. Lau isingejumuisha, basi kusingehitajika kuuwekea kizuizi pale inapokusudiwa aina maalumu. Kwa ujumla lugha na desturi ziko juu ya kwamba soksi ni kila kinachovaliwa mguuni bila ngozi, ni mamoja kiwe na soli au kisiwe nacho. Miongoni mwa mambo yanayotambulika vyema ni kwamba kila jina lililotajwa wazi ndani ya Qur-aan au Sunnah na likafungamanishwa nalo hukumu miongoni mwa hukumu, basi ni lazima hukumu hiyo iwekwe tu juu ya kile kinachopelekea jina hilo na isivushwe nje ya matumizi yake ya Kishari´ah.
- Muhusika: ´Allaamah Muhammad Jamaal-ud-Diyn bin Muhammad al-Qaasimiy (afk. 1332)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Mash ´alaal-Jawrabayn, uk. 51-52
- Imechapishwa: 09/04/2026
Mfano wa soksi hauhitaji kuungwa mkono maana yake ya kilugha na ya Kishari´ah. Inajulikana kwa kila mtu kutokana na nukuu za wanazuoni kuhusu maana yake, kwa sababu hilo ni katika mlango wa kufafanua yaliyo wazi. Lakini kilichotulazimisha kufanya hivyo ni yale tuliyoyaona katika baadhi ya vitabu vya wale waliodai kwamba soksi ni soksi za ngozi zinazovaliwa juu ya soksi za ngozi hadi kwenye vifundo kwa ajili ya baridi na kulinda soksi za ngozi ya chini dhidi ya uchafu na maji ya kuosha. Mwingine akaifungamanisha na kuwa ni ya ngozi. Haya ni makosa katika lugha, desturi na Fiqh pia, kwa sababu kinachodaiwa hapo ni buti na si soksi. Cha kushangaza ni maneno ya al-Jazuuliy miongoni mwa wanazuoni wa Maalikiyyah:
”Wametofautiana kuhusu soksi na vuti na kama ni vitu viwili tofauti au ni kitu kimoja.”
Chanzo cha tofauti hiyo ni yale yaliyopokewa katika ”at-Tawdhwiyh” ya kwamba Imaam Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) alitafsiri buti kuwa ni soksi iliotiwa ngozi chini na juu, basi wakadhania kutokana na hilo kwamba soksi haiwi isipokuwa hivyo tu, ilihali soksi ikiwekewa ngozi kwa sifa hiyo na kuitwa buti, haimaanishi kuwa kila soksi ni buti, kwa sababu soksi hujumuisha yenye ngozi na isiyokuwa na ngozi. Lau isingejumuisha, basi kusingehitajika kuuwekea kizuizi pale inapokusudiwa aina maalumu. Kwa ujumla lugha na desturi ziko juu ya kwamba soksi ni kila kinachovaliwa mguuni bila ngozi, ni mamoja kiwe na soli au kisiwe nacho. Miongoni mwa mambo yanayotambulika vyema ni kwamba kila jina lililotajwa wazi ndani ya Qur-aan au Sunnah na likafungamanishwa nalo hukumu miongoni mwa hukumu, basi ni lazima hukumu hiyo iwekwe tu juu ya kile kinachopelekea jina hilo na isivushwe nje ya matumizi yake ya Kishari´ah.
Muhusika: ´Allaamah Muhammad Jamaal-ud-Diyn bin Muhammad al-Qaasimiy (afk. 1332)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Mash ´alaal-Jawrabayn, uk. 51-52
Imechapishwa: 09/04/2026
https://firqatunnajia.com/28-kila-mtu-anajua-soksi-ni-nini/