Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
172 – Hii ndio dini na ´Aqiydah yetu, kwa nje na kwa ndani.
173 – Sisi tunajitenga mbali kutokana na ambaye anaenda kinyume na yale yote tuliyoyataja na kuyabainisha.
174 – Tunamuomba Allaah (Ta´ala) atuthibitishe juu ya imani na atufishe katika hali hiyo.
MAELEZO
Yote tuliyoyataja katika kitabu hichi cha ´Aqiydah ndio dini yetu sisi waislamu. Sisi tunajitenga mbali na kila ambaye anaenda kinyume nayo. Kwa sababu ni ´Aqiydah ya haki na yale yote yanayoenda kinyume nayo ni ya batili.
Baada ya mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) kubainisha ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah, akafanya adabu na Allaah na akamuomba amfanye imara juu yake. Haitoshi kwa mtu akaitambua ´Aqiydah. Mwanachuoni anaweza kutekeleza na kukosea. Kamwe mtu asidanganyike kwa elimu yake na akajihisi salama kutokana na mitihani. Je, elimu yake inalingana na elimu ya Ibraahiym (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Yeye ndiye alisema:
رَبِّ اجْعَلْ هَـٰذَا الْبَلَدَ آمِنًا وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ
“Ibraahiym aliposema: “Ee Mola wangu! Ufanye mji huu uwe wa amani na unikinge mimi na wanangu kuabudu masanamu.” Ee Mola wangu! Hakika hao wamepoteza wengi kati ya watu.”[1]
Mtu anatakiwa kumuomba Allaah usalama. Ni wanazuoni wangapi wametekeleza na kupinda kutokana na dini! Matendo yanazingatiwa ule mwisho wake.
[1] 14:35-36
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 262-263
- Imechapishwa: 27/05/2025
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
172 – Hii ndio dini na ´Aqiydah yetu, kwa nje na kwa ndani.
173 – Sisi tunajitenga mbali kutokana na ambaye anaenda kinyume na yale yote tuliyoyataja na kuyabainisha.
174 – Tunamuomba Allaah (Ta´ala) atuthibitishe juu ya imani na atufishe katika hali hiyo.
MAELEZO
Yote tuliyoyataja katika kitabu hichi cha ´Aqiydah ndio dini yetu sisi waislamu. Sisi tunajitenga mbali na kila ambaye anaenda kinyume nayo. Kwa sababu ni ´Aqiydah ya haki na yale yote yanayoenda kinyume nayo ni ya batili.
Baada ya mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) kubainisha ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah, akafanya adabu na Allaah na akamuomba amfanye imara juu yake. Haitoshi kwa mtu akaitambua ´Aqiydah. Mwanachuoni anaweza kutekeleza na kukosea. Kamwe mtu asidanganyike kwa elimu yake na akajihisi salama kutokana na mitihani. Je, elimu yake inalingana na elimu ya Ibraahiym (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Yeye ndiye alisema:
رَبِّ اجْعَلْ هَـٰذَا الْبَلَدَ آمِنًا وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ
“Ibraahiym aliposema: “Ee Mola wangu! Ufanye mji huu uwe wa amani na unikinge mimi na wanangu kuabudu masanamu.” Ee Mola wangu! Hakika hao wamepoteza wengi kati ya watu.”[1]
Mtu anatakiwa kumuomba Allaah usalama. Ni wanazuoni wangapi wametekeleza na kupinda kutokana na dini! Matendo yanazingatiwa ule mwisho wake.
[1] 14:35-36
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 262-263
Imechapishwa: 27/05/2025
https://firqatunnajia.com/240-haitoshi-kuitambua-aqiydah-sahihi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
