Nilisikia jinsi ambavyo Abu ´Aliy al-Hasan bin Safwaan al-Bardha´iy anavyosomewa katika Rajab mwaka wa 338: Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin ´Ubayd bin Sufyaan bin Abiyd-Dunyaa al-Qurashiy (Rahimahu Allaah) ametuhadithia:
128 – Sa´duuyah ametuhadithia, kutoka kwa ´Abbaad bin al-´Awwaam, kutoka kwa Muhammad bin Ishaaq, kutoka kwa ´Abdullaah bin Abiy Umaamah, kutoka kwa Ka´b bin Maalik, kutoka kwa baba yake, aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Uchakavu ni katika imani.”[1]
129 – Haaruun bin ´Abdillaah ametuhadithia: Ma´n ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Muniyb bin ´Abdillaah bin Abiy Umaamah al-Answaariy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Mahmuud bin Labiyd, kutoka kwa Abu Umaamah al-Answaariy, ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Uchakavu ni katika imani.”
Haaruun amesema:
”Nilimuuliza Ma´n nini maana ya uchakavu. Akasema: ”Ni vazi lililo chini ya ubora wa vazi jingine.”
Akimaanisha vazi la chini.
130 – Yahyaa bin Ayyuub ametuhadithia: ´Aliy bin Haashim ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Zayd bin Wahb, ambaye ameeleza:
”Nilimuona ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) ametoka kwenda sokoni akiwa na fimbo mkononi mwake na akiwa amevaa kikoi chenye viraka kumi na vinne, ambapo baadhi yake vikiwa vya ngozi.”
131 – Shu´ayb bin Harb ametuhadithia, kutoka kwa Sulaymaan bin al-Mughiyrah, kutoka kwa Thaabit, kutoka kwa Anas, aliyesema:
”Niliona kati ya mabega ya ´Umar (Rahimahu Allaah) viraka vinne.”
132 – Surayj bin Yuunus amenihadithia: ´Aliy bin Haashim ametuhadithia, kutoka kwa Ismaa´iyl al-Bazzaar, kutoka kwa Umm ´Afiyf, ambaye ameeleza:
”Nilimuona ´Aliy bin Abiy Twaalib amevaa shuka nyekundu miongoni mwa mashuka ya wabebaji mizigo, ikiwa na kiraka cheupe.”
133 – Khalaf bin Saalim ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa ´Amr bin Qays, ambaye amesema:
”´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) alionekana amevaa kikoi chenye viraka, akakemewa kwa vazi lake hilo, akasema: ”waumini wataiga kwa hili na moyo utanyenyekea kwa hili.”
134 – al-Fadhwl bin Sahl amenihadithia: Abu Nu´aym ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia, kutoka kwa al-Ajlah, kutoka kwa ´Abdullaah bin Abiyl-Hudhayl, ambaye amesema:
”Nilimuona ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) amevaa kanzu ya zamani sana iliyokuwa ikikaribia kuchakaa, ikiposhikiliwa ilifikia kucha na ikiachwa ilifika katikati ya mkono.”
[1] Abu Daawuud (4161). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (4161).
- Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 167-177
- Imechapishwa: 04/02/2026
Nilisikia jinsi ambavyo Abu ´Aliy al-Hasan bin Safwaan al-Bardha´iy anavyosomewa katika Rajab mwaka wa 338: Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin ´Ubayd bin Sufyaan bin Abiyd-Dunyaa al-Qurashiy (Rahimahu Allaah) ametuhadithia:
128 – Sa´duuyah ametuhadithia, kutoka kwa ´Abbaad bin al-´Awwaam, kutoka kwa Muhammad bin Ishaaq, kutoka kwa ´Abdullaah bin Abiy Umaamah, kutoka kwa Ka´b bin Maalik, kutoka kwa baba yake, aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Uchakavu ni katika imani.”[1]
129 – Haaruun bin ´Abdillaah ametuhadithia: Ma´n ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Muniyb bin ´Abdillaah bin Abiy Umaamah al-Answaariy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Mahmuud bin Labiyd, kutoka kwa Abu Umaamah al-Answaariy, ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Uchakavu ni katika imani.”
Haaruun amesema:
”Nilimuuliza Ma´n nini maana ya uchakavu. Akasema: ”Ni vazi lililo chini ya ubora wa vazi jingine.”
Akimaanisha vazi la chini.
130 – Yahyaa bin Ayyuub ametuhadithia: ´Aliy bin Haashim ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Zayd bin Wahb, ambaye ameeleza:
”Nilimuona ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) ametoka kwenda sokoni akiwa na fimbo mkononi mwake na akiwa amevaa kikoi chenye viraka kumi na vinne, ambapo baadhi yake vikiwa vya ngozi.”
131 – Shu´ayb bin Harb ametuhadithia, kutoka kwa Sulaymaan bin al-Mughiyrah, kutoka kwa Thaabit, kutoka kwa Anas, aliyesema:
”Niliona kati ya mabega ya ´Umar (Rahimahu Allaah) viraka vinne.”
132 – Surayj bin Yuunus amenihadithia: ´Aliy bin Haashim ametuhadithia, kutoka kwa Ismaa´iyl al-Bazzaar, kutoka kwa Umm ´Afiyf, ambaye ameeleza:
”Nilimuona ´Aliy bin Abiy Twaalib amevaa shuka nyekundu miongoni mwa mashuka ya wabebaji mizigo, ikiwa na kiraka cheupe.”
133 – Khalaf bin Saalim ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa ´Amr bin Qays, ambaye amesema:
”´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) alionekana amevaa kikoi chenye viraka, akakemewa kwa vazi lake hilo, akasema: ”waumini wataiga kwa hili na moyo utanyenyekea kwa hili.”
134 – al-Fadhwl bin Sahl amenihadithia: Abu Nu´aym ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia, kutoka kwa al-Ajlah, kutoka kwa ´Abdullaah bin Abiyl-Hudhayl, ambaye amesema:
”Nilimuona ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) amevaa kanzu ya zamani sana iliyokuwa ikikaribia kuchakaa, ikiposhikiliwa ilifikia kucha na ikiachwa ilifika katikati ya mkono.”
[1] Abu Daawuud (4161). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (4161).
Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 167-177
Imechapishwa: 04/02/2026
https://firqatunnajia.com/19-unyenyekevu-katika-mavazi/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket