Yanatosha haya. Nimeacha Hadiyth zingine nyingi zinazofahamisha uwekwaji Shari´ah wa kupangusa juu ya viatu ikiwa ni pamoja na katika “Majma´-uz-Zawaa’id” na “al-Musannaf” ya ´Abdur-Razzaaq, kwa sababu ya usahihi wake ingawa baadhi yazo zinafaa kutumiwa kwa lengo la kutilia nguvu na ufuatiliaji. Khaswa ukizingatia kuwa at-Twahaawiy amesema kuwa Hadiyth zinazojulisha kufaa kuswali na viatu zimepokelewa kwa mapokezi tele. Amesema:
”Kumesimuliwa Hadiyth nyingi mno kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) zinazoonyesha kuwa kuswali na viatu ni jambo limewekwa katika Shari´ah. Zinafahamisha kuanzia kwamba yeye mwenyewe (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali na viatu vyake na akavua viatu vyake kwa sababu ya uchafu, mpaka kuruhusu kuswali na viatu.”[1]
Wanazuoni hawashurutishi kuwa kila njia ya Hadiyth iwe Swahiyh au nzuri ili Hadiyth izingatiwe kuwa imepokelewa kwa mapokezi mengi. Bali wanajumuisha zilizokuwa Swahiyh, nzuri na dhaifu.
[1] Ma´aaniyl-Aathaar (1/511).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 17
- Imechapishwa: 03/06/2025
Yanatosha haya. Nimeacha Hadiyth zingine nyingi zinazofahamisha uwekwaji Shari´ah wa kupangusa juu ya viatu ikiwa ni pamoja na katika “Majma´-uz-Zawaa’id” na “al-Musannaf” ya ´Abdur-Razzaaq, kwa sababu ya usahihi wake ingawa baadhi yazo zinafaa kutumiwa kwa lengo la kutilia nguvu na ufuatiliaji. Khaswa ukizingatia kuwa at-Twahaawiy amesema kuwa Hadiyth zinazojulisha kufaa kuswali na viatu zimepokelewa kwa mapokezi tele. Amesema:
”Kumesimuliwa Hadiyth nyingi mno kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) zinazoonyesha kuwa kuswali na viatu ni jambo limewekwa katika Shari´ah. Zinafahamisha kuanzia kwamba yeye mwenyewe (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali na viatu vyake na akavua viatu vyake kwa sababu ya uchafu, mpaka kuruhusu kuswali na viatu.”[1]
Wanazuoni hawashurutishi kuwa kila njia ya Hadiyth iwe Swahiyh au nzuri ili Hadiyth izingatiwe kuwa imepokelewa kwa mapokezi mengi. Bali wanajumuisha zilizokuwa Swahiyh, nzuri na dhaifu.
[1] Ma´aaniyl-Aathaar (1/511).
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 17
Imechapishwa: 03/06/2025
https://firqatunnajia.com/17-hadiyth-kwa-mapokezi-mengi-kuhusu-kusuniwa-kuswali-na-viatu/