116 – ´Abdullaah bin Abiy Badr ametuhadithia: Shu´ayb bin Harb ametukhabarisha: Swaalih al-Murriy ametuhadithia:

”Alitoka al-Hasan, Yuunus na Ayyuub na huku wakikumbushana kuhusu unyenyekevu. al-Hasan akawaambia: “Je, mnajua unyenyekevu ni nini? Unyenyekevu ni kutoka nyumbani kwako na usikutane na muislamu yeyote isipokuwa umuone kuwa ni mbora kuliko wewe.”

117 – Ishaaq bin Ibraahiym ametuhadithia: Abu Yaziyd ar-Raaziy ametuhadithia: Ishaaq bin Ibraahiym bin Yaziyd ametuhadithia: Maslamah bin Ja´far ametuhadithia, kutoka kwa Sa´d at-Twaa’iy, aliyeeleza kwamba Iysaa bin Maryam (´alayhis-Salaam) amesema:

”Twubaa kwa wanyenyekevu duniani, hao ndio wenye viti vya nuru siku ya Qiyaamah. Twubaa kwa wanaotengeneza baina ya watu duniani, hao ndio warithi wa al-Firdaws siku ya Qiyaamah. Twubaa kwa waliotwaharika nyoyo zao duniani, hao ndio wataomuona Allaah (´Azza wa Jall) siku ya Qiyaamah.”

118 – Ahmad bin Hanbal ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Mubaarak ametukhabarisha: al-Mas´uudiy ametukhabarisha, kutoka kwa Yahyaa bin Kathiyr, ambaye amesema:

“Asili ya unyenyekevu ni mambo matatu: Kuridhika na sehemu ya chini ya kikao, kuanza kwa salamu kwa yule unayekutana naye na kuchukia kusifiwa na kujionyesha kwa wema.”

119 – Kwa njia hiyohiyo ametukhabarisha Ma´mar: Yuunus bin Khabbaab amenikhabarisha, kutoka kwa Mujaahid, ambaye amesema:

“Hakika Allaah (´Azza wa Jall) alipowazamisha watu wa Nuuh, basi milima ilijivuna na mlima al-Juwdiy ukanyenyekea, Allaah akauinua juu ya milima na akaufanya kuwa ndio mahala pa kupumzika kwa safina.”

120 – Kutokea huko ametuhadithia Hamzah bin Najiyd, kutoka kwa Salamah bin Abiy Habiyb, kutoka kwa ´Abdullaah bin al-Hasan, ambaye ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Anayenyenyekea Allaah humuinua, anayejivuna Allaah humvunja, anayejitegemea Allaah humtajirisha, anayebadhirisha Allaah humfakirisha na anayemtaja Allaah (´Azza wa Jall) Allaah humpenda.”[1]

121 – Kwa njia hiyohiyo ametuhadithia Zakariyyaa bin ´Adiy, kutoka kwa Yahyaa bin Sulaym at-Twaa’iy, kutoka kwa Muhammad bin ´Abdillaah bin ´Amr bin ´Uthmaan: Nimefikiwa ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Anapomuongoza Allaah kwa Uislamu mja, akapendezesha sura yake, akamweka katika nafasi isiyomfedhehesha na akamruzuku pamoja na hayo unyenyekevu, basi huyo ni miongoni mwa waliochaguliwa na Allaah (´Azza wa Jall).”

122 – Muhammad bin ´Abdillaah bin Muusa amenihadithia: Zayd bin Hubaab ametuhadithia, kutoka kwa Shu´bah, kutoka kwa ´Aliy bin Zayd, kutoka kwa Anas bin Maalik, ambaye amesema:

“Hakika kijakazi wa mjini Madiynah alikuwa akimshika mkono Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) naye hasiti kuufuta mkono wake mpaka ampeleke popote apendapo.”[2]

[1] al-Haythamiy amesema:

“Kwa njia hiyohiyo nazitambua mbili tu.” (Madjma´-uz-Zawaa’id (10/253))

[2] Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan Ibn Maajah” (3386).

  • Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 152-158
  • Imechapishwa: 04/02/2026