Ibn Maajah amesimulia kutoka kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye amesimulia:
“Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam), macho yake hayatoki miguu yake. Baadaye akafa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali, macho yake hayaachi paji lake la uso. Baadaye akafa Mtume wa Allaah (Radhiya Allaahu ´anh). Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali, macho yake hayaachi mahali kilipo Qiblah. Baadaye akafa ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) na kukazuka fitina. Hapo ndipo watu wakawa wanatazama kuliani na kushotoni.”[1]
´Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anhaa) alimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kuhusu kugeuka kuliani na kushotoni wakati wa kuswali, akasema:
“Ni wizi ambao shaytwaan huiba kutoka kwenye swalah ya mja.”[2]
[1] Ibn Maajah (1634). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (294).
[2] al-Bukhaariy (751).
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Hanbaliy (afk. 795)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Khushuu´ fiys-Swalaah, uk. 70-71
- Imechapishwa: 24/11/2025
Ibn Maajah amesimulia kutoka kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye amesimulia:
“Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam), macho yake hayatoki miguu yake. Baadaye akafa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali, macho yake hayaachi paji lake la uso. Baadaye akafa Mtume wa Allaah (Radhiya Allaahu ´anh). Wakati mtu alipokuwa akisimama kuswali, macho yake hayaachi mahali kilipo Qiblah. Baadaye akafa ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) na kukazuka fitina. Hapo ndipo watu wakawa wanatazama kuliani na kushotoni.”[1]
´Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anhaa) alimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kuhusu kugeuka kuliani na kushotoni wakati wa kuswali, akasema:
“Ni wizi ambao shaytwaan huiba kutoka kwenye swalah ya mja.”[2]
[1] Ibn Maajah (1634). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (294).
[2] al-Bukhaariy (751).
Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Hanbaliy (afk. 795)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Khushuu´ fiys-Swalaah, uk. 70-71
Imechapishwa: 24/11/2025
https://firqatunnajia.com/16-mitihani-inaondosha-unyenyekevu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
