al-Qummiy amesema:
”Ahmad bin Muhammad ametuhadithia, kutoka kwa Ja´far bin ´Abdillaah, kutoka kwa Kathiyr bin ´Ayyaash, kutoka kwa Abul-Jaaruud, kutoka kwa Abu Ja´far ambaye amesema kuhusiana na maneno Yake:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ
“Enyi walioamini! Muitikieni Allaah na Mtume anapokuiteni katika yale yenye kukuhuisheni!”[1]
Amesema: “Inamaanisha uongozi wa ´Ali bin Abiy Twaalib. Kwani kumfuata yeye na kumkubali kama kiongozi kunaleta umoja miongoni mwenu na kulinda uadilifu kwenu.”[2]
Allaah amemtakasa Abu Ja’far kutokana na uongo huu na upotoshaji. Angalia jinsi wanavyokusudia kufuta maana za Aayah za Qur-aan na kubatilisha ujumla wake.
Kinachokusudiwa na yale yanayowapa watu uhai ni Uislamu ambao uliletwa na Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ukiwa na imani zake, ´ibaadah, maadili, miamala, jihaad, kuamrisha mema na kukataza maovu. Aayah haimaanishi, kwa namna yoyote ile, madai haya ya uongo yaliyobuniwa na huyu Baatwiniy.
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hajawahi kamwe kuhubiri uongozi huu wa kufikirika uliobuniwa na Ibn Saba´, ambao Baatwiniy na Raafidhwah wakaenda kuufanyia kazi kwa ajili ya kukengeusha sehemu kubwa ya Aayah za Qur-aan kwa sababu yake.
[1] 8:24
[2] Tafsiyr al-Qummiy (1/271).
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 219
- Imechapishwa: 13/08/2025
al-Qummiy amesema:
”Ahmad bin Muhammad ametuhadithia, kutoka kwa Ja´far bin ´Abdillaah, kutoka kwa Kathiyr bin ´Ayyaash, kutoka kwa Abul-Jaaruud, kutoka kwa Abu Ja´far ambaye amesema kuhusiana na maneno Yake:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ
“Enyi walioamini! Muitikieni Allaah na Mtume anapokuiteni katika yale yenye kukuhuisheni!”[1]
Amesema: “Inamaanisha uongozi wa ´Ali bin Abiy Twaalib. Kwani kumfuata yeye na kumkubali kama kiongozi kunaleta umoja miongoni mwenu na kulinda uadilifu kwenu.”[2]
Allaah amemtakasa Abu Ja’far kutokana na uongo huu na upotoshaji. Angalia jinsi wanavyokusudia kufuta maana za Aayah za Qur-aan na kubatilisha ujumla wake.
Kinachokusudiwa na yale yanayowapa watu uhai ni Uislamu ambao uliletwa na Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ukiwa na imani zake, ´ibaadah, maadili, miamala, jihaad, kuamrisha mema na kukataza maovu. Aayah haimaanishi, kwa namna yoyote ile, madai haya ya uongo yaliyobuniwa na huyu Baatwiniy.
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hajawahi kamwe kuhubiri uongozi huu wa kufikirika uliobuniwa na Ibn Saba´, ambao Baatwiniy na Raafidhwah wakaenda kuufanyia kazi kwa ajili ya kukengeusha sehemu kubwa ya Aayah za Qur-aan kwa sababu yake.
[1] 8:24
[2] Tafsiyr al-Qummiy (1/271).
Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 219
Imechapishwa: 13/08/2025
https://firqatunnajia.com/159-al-qummiy-upotoshaji-wake-wa-tatu-wa-al-anfaal/