al-Haakim (1/139) amesema: Muhammad bin Swaalih na Ibraahiym bin ´Iswmah ametuhadithia: as-Sarriy bin Khuzaymah ametuhadithia: Muusa bin Ismaa´iyl ametuhadithia … Vilevile Abul-Waliyd al-Faqiyh ametufahamisha: al-Hasan bin Sufyaan ametuhadithia: Ibraahiym bin al-Hajjaaj ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Muthannaa al-Answaariy ametuhadithia, kutoka kwa Thumaamah, kutoka kwa Anas, ambaye ameeleza:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwahi kuvua viatu vyake wakati wa swalah isipokuwa mara moja tu, ambapo alivua na watu nao wakavua. Akasema: ”Mna nini nyinyi?” Wakasema: ”Umevua nasi tukavua.” Akasema: ”Jibriyl amekuja na kunijulisha kuwa vina uchafu.”
al-Haakim amesema:
”Hadiyth ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy. Amesimulia kutoka kwa ´Abdullaah bin al-Muthannaa kwa lengo la kumjengea hoja. Si al-Bukhaariy wala Muslim hakuna aliyeikpokea.”
adh-Dhahabiy ameafikiana naye.
Haafidhw al-Haythamiy amesema:
“Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Wanaume wake ni wanaume Swahiyh. al-Bazzaar ameipokea kwa toleo fupi.”[1]
[1] Majma´-uz-Zawaa’id (2/56).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 15-16
- Imechapishwa: 03/06/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket