12. Hadiyth “Mkimuona mwenye kununua au kuuza msikitini… “

291 – Amesimulia tena ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

إذا رأيتم من يبيعُ أو يبتاع في المسجد، فقولوا: لا أربح الله تجارتك، وإذا رأيتم من ينشد ضالة، فقولوا: لا ردها الله عليك

“Mkimuona mwenye kununua au kuuza msikitini, basi semeni: “Allaah asiipe faida biashara yako!” Na mkimuona mwenye kumtangaza mnyama wake aliyepotea, basi semeni: “Allaah asikuridhie naye!”[1]

Ameipokea at-Tirmidhiy na akasema:

“Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”

Ameipokea vilevile an-Nasaa’iy, Ibn Khuzaymah na al-Haakim ambaye amesema:

“Ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za Muslim.”

Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” amepokea Hadiyth nusu ya kwanza mfano wake.

[1] Swahiyh.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/236-237)
  • Imechapishwa: 16/11/2022
  • Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy