Mimi nampa changamoto kwa mwenye kusema kuwa Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab ameleta madhehebu mapya. Ninampa changamoto alete madhehebu hayo na atubainishie nayo.

Mimi nampa changamoto mwenye kusema kuwa Shaykh anawakufurisha waislamu.

Nampa changamoto mwenye kusema kuwa Shaykh aliua muislamu mmoja, sembuse mwenye kusema kuwa aliua waislamu.

Ninampa changamoto mwenye kusema kuwa Shaykh anawakufurisha waislamu. Badala yake Shaykh anawakufurisha waabudu makaburi. Watu hawa wamekufurishwa na Qur-aan, Sunnah na maafikiano ya wanazuoni. Kubwa liliopo ni kuwa Shaykh alifanya kazi hii, akawa, subira na kutaraji malipo kutoka kwa Allaah ilihali wanazuoni wengine walinyamaza na kula raha.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Radd Shubuhaat hawl Da´wat-il-Mujaddid, uk. 56-57
  • Imechapishwa: 08/02/2026