Imaam al-Barbahaariy (Rahimahu Allaah) amesema:
na ni Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Yule asiyechukua kutoka kwao amepotea na kuzusha. Kila Bid´ah ni upotevu na upotevu na watu wake ni Motoni.
Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wale waliokuja baada yao ambao wamewafuata kwa wema ndio Ahl-us-Sunnah. Hawa ndio watu wenye kufuata njia sahihi. Hii ndio Sunnah anayopambanua hivi sasa. Nao vilevile ndio al-Jamaa´ah ya kihakika. Kuhusu kukusanyika kwa wengine juu ya mambo batili, hawa hawastahiki kuitwa al-Jamaa´ah. Haijalishi kitu hata kama itakuwa ni idadi ya watu wengi:
تَحْسَبُهُمْ جَمِيعًا وَقُلُوبُهُمْ شَتَّىٰ
”Utawadhania wako pamoja, kumbe nyoyo zao ziko mbalimbali.” (59:14)
Wao sio al-Jamaa´ah. al-Jamaa´ah ni wale walio juu ya haki. Hawa ndio al-Jamaa´ah.
Ambaye anasema kuwa yeye anafuata kipote fulani na ndio al-Jamaa´ah. Nyinyi mnasema tulazimiane na al-Jamaa´ah na hawa ninaowafuata ndio al-Jamaa´ah. Tunawauliza nani kasema kuwa hawa ndio Jamaa´ah? al-Jamaa´ah ni wale walio katika haki na juu ya Sunnah. Hawa ndio al-Jamaa´ah.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Sharh-is-Sunnah, uk. 19
- Imechapishwa: 01/10/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)