Kwa mnasaba wa Aayah hii napendezwa na yale yaliyothibiti kwa Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´an) ambapo alijiwa na mwanamke na kumwambia: “Wewe ndiye unayesema: “Allaah amewalaani wenye kuwanyoa wenzao nyusi na wenye kunyolewa, wenye kuwachanja[1] wenzao… ?” Akajibu: “Ndio.” Mwanamke yule akasema: “Mimi nimesoma Kitabu cha Allaah chote kuanzia mwanzo mpaka mwisho na sijapata hicho unachokisema.” Akamwambia mwanamke yule: “Ikiwa kweli umefanya hivo basi umepata. Je, hivi hukusoma:
وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا
“Kile alichokupeni Mtume, basi kichukueni, na kile anachokukatazeni, basi kiacheni.”?
Akajibu: “Ndio.” Ibn Mas´uud akamwambia: “Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema: “Allaah amewalaani wenye kuwachanja wenzao… “
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[1] Tattoo.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manzilat-us-Sunnah fiyl-Islaam, uk. 14-15
- Imechapishwa: 10/02/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket