Katika siku hizi kuna matendo yenye fadhilah nyingi na utiifu mwingi ikiwa ni pamoja na:
1 – Kuzidisha swalah za Sunnah, swadaqah na matendo mengine mema kama kuwafanyia wema wazazi, kuunga ukoo, tawbah ya kweli na kurejea kwa Allaah kwa unyenyekevu.
2 – Kuzidisha kumtaja Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kusema ”Allaahu Akbar” na kusoma Qur-aan.
3 – Funga. Hata kama hakuna Hadiyth maalum inayohusisha funga ya siku tisa za Dhul-Hijjah, lakini kufunga ni miongoni mwa matendo bora yaliyohimizwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa hivyo inapata kufahamika kuwa kufunga siku hiyo ni jambo linalopendeza kutokana na dalili za jumla.
4 – Kufanya Hajj na ´Umrah, ambayo ni miongoni mwa matendo bora kabisa, kama itakavyokuja – Allaah akitaka.
5 – Kufanya bidii kuchinja Udhhiyah na kutolichukulia jambo hili kwa wepesi, kwa sababu ya ujira wake mkubwa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 6-7
- Imechapishwa: 04/05/2025
Katika siku hizi kuna matendo yenye fadhilah nyingi na utiifu mwingi ikiwa ni pamoja na:
1 – Kuzidisha swalah za Sunnah, swadaqah na matendo mengine mema kama kuwafanyia wema wazazi, kuunga ukoo, tawbah ya kweli na kurejea kwa Allaah kwa unyenyekevu.
2 – Kuzidisha kumtaja Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kusema ”Allaahu Akbar” na kusoma Qur-aan.
3 – Funga. Hata kama hakuna Hadiyth maalum inayohusisha funga ya siku tisa za Dhul-Hijjah, lakini kufunga ni miongoni mwa matendo bora yaliyohimizwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa hivyo inapata kufahamika kuwa kufunga siku hiyo ni jambo linalopendeza kutokana na dalili za jumla.
4 – Kufanya Hajj na ´Umrah, ambayo ni miongoni mwa matendo bora kabisa, kama itakavyokuja – Allaah akitaka.
5 – Kufanya bidii kuchinja Udhhiyah na kutolichukulia jambo hili kwa wepesi, kwa sababu ya ujira wake mkubwa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 6-7
Imechapishwa: 04/05/2025
https://firqatunnajia.com/03-mfano-wa-matendo-mema-yanayofanywa-katika-kumi-la-kwanza-la-dhul-hijjah/