وأول ما فرض الله على عباده الكفر بالطاغوت والإيمان بالله، قال تعالى
Kitu cha kwanza Allaah kukifaradhisha kwa waja ni kukufuru Twaaghuut na kumuamini Allaah. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ
“Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Mtume [awaamrishe watu wake] kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaaghuut.”[1]
والطاغوت: ما عبد من دون الله أو الشيطان، والطاغوت، والكهانة، والمنجم، ومن يحكم بغير ما أنزل الله، وكل متبوع مطاع على غير الحق
Twaaghuut ni:
1- Kila chenye kuabudiwa badala ya Allaah.
2- Shaytwaan.
3- Kuhani.
4- Mnajimu.
5- Anayehukumu kinyume na aliyoteremsha Allaah.
6- Kila mwenye kufuatwa na kutiiwa katika kitu kisichokuwa haki.
قال العلامة ابن القيم رحمه الله تعالى: الطاغوت: ما يجاوز به العبد حده من معبود، أو متبوع، أو مطاع
´Allaamah Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:
“Twaaghuut ni kila chenye kuabudiwa, kufuatwa na kutiiwa ambacho mja amepindukia kwacho mipaka.”[2]
[1] 16:36
[2] I´laam-ul-Muwaqqi´iyn (1/5).
- Muhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´liym-us-Swibyaan at-Tawhiyd, uk. 15-16
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)