02. Mtume akiomba msamaha kwa siku mara mia

22al-Agharr bin Yasaar al-Muzaniy (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Enyi watu! Tubuni kwa Allaah. Kwani hakika mimi natubia Kwake mara mia kwa siku.”[1]

Ameipokea Muslim.

23 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

“Naapa kwa Allaah! Hakika mimi namwomba Allaah msamaha na kutubia Kwake kwa siku zaidi ya mara sabini.”[2]

Ameipoke al-Bukhaariy.

MAELEZO

Hadiyth hizi mbili kuna kusuniwa kuomba msamaha na kutubu. Ikiwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaomba msamaha katika kikao kimoja mara mia, ilihali Allaah amekwishamsamehe madhambi yake yaliyotangulia na yatayokuja huko mbele, tusemeje sisi?

Hakika mambo yalivyo ni kwamba yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo – ilihali Allaah amekwishamsamehe madhambi yake yaliyotangulia na yatayokuja huko mbele – kwa ajili ya kumwabudu Allaah, kumshukuru na ili ummah waweze kumuigiliza yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

[1] Muslim (2702).

[2] al-Bukhaariy (6307).

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 28
  • Imechapishwa: 05/10/2025