Jina la “Allaah” ni ufahamisho wa dhati tukufu. Hakuna mwengine mwenye kuitwa hivo zaidi Yake (Subhaanahu wa Ta´ala). Hata wajeuri na makafiri hawajiiti hivo. Hakuna mwenye kujiita “Allaah”. Fir´awn alisema:
فأَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ
“Mimi ni mola wenu mkuu.”[1]
Hakusema kuwa yeye ni Allaah. Pamoja na ukafiri wake hakuwa na ujasiri wa kujiita jina hilo. Ni jina maalum kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
Jina “Allaah” maana yake ni “Yule mwenye uungu”, bi maana mwenye kuabudiwa. Viumbe wote wanawajibika kumwabudu Yeye, kama alivosema Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa)[2].
[1] 79:24
[2] Jaami´-ul-Bayaan (1/45).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 20
- Imechapishwa: 06/08/2019
Jina la “Allaah” ni ufahamisho wa dhati tukufu. Hakuna mwengine mwenye kuitwa hivo zaidi Yake (Subhaanahu wa Ta´ala). Hata wajeuri na makafiri hawajiiti hivo. Hakuna mwenye kujiita “Allaah”. Fir´awn alisema:
فأَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ
“Mimi ni mola wenu mkuu.”[1]
Hakusema kuwa yeye ni Allaah. Pamoja na ukafiri wake hakuwa na ujasiri wa kujiita jina hilo. Ni jina maalum kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
Jina “Allaah” maana yake ni “Yule mwenye uungu”, bi maana mwenye kuabudiwa. Viumbe wote wanawajibika kumwabudu Yeye, kama alivosema Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa)[2].
[1] 79:24
[2] Jaami´-ul-Bayaan (1/45).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 20
Imechapishwa: 06/08/2019
https://firqatunnajia.com/02-maana-ya-neno-allaah/