Swali 373: Ni ipi hukumu kuhusu ndoa kwa nia ya kuacha?
Jibu: Haya nimeyapata kwenye fatwa ya Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah na anasema akimuoa mwanamke kisha wakati anaporejea kutoka katika mji ule akamwacha ndoa hiyo imechukizwa. Kwani imefanana na Mut´ah. Kinachonidhihirikia ni kwamba muislamu anatakiwa kujiepusha nayo kwa sababu isije kuwa ni aina fulani ya Mut´ah. Kwani ndoa hiyo imekaribia maana ya Mut´ah. Rejeeni masuala hayo katika “Majmuu´-ul-Fataawaa” ya Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah katika mjeledi maalum unaozungumzia ndoa. Kimbilia kujiepusha na mambo yenye utata.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 627
- Imechapishwa: 08/12/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket