Swali: Nina wafanyakazi wenzangu hawaswali na nimewanasihi mara nyingi lakini hawajakubali nasaha. Nifanye nini?

Jibu: Peleka jambo lao kwa chombo kinachohusika na kinachosimamia kazi na uwajulishe kwamba wanakosa swalah ya mkusanyiko, peleka jambo lao kwa mamlaka husika, kwa kiongozi wa mji au kwa mahakama. Unapaswa kujitahidi katika mambo yatakayosaidia kuwaongoza. Huenda Allaah akawaongoza kwa sababu zako. Anza kwa kuwajulisha anayewasimamia. Huenda Allaah akamsaidia kuwanasihi, kuwaelekeza na kuwalazimisha kushikamana na haki.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/189)
  • Imechapishwa: 24/02/2026