Swali: Je, ni lazima kufanya uadilifu kati ya wake wawili baina yao katika safari?
Jibu: Ni wajibu awe mwadilifu baina yao katika safari kwa maridhiano au kwa kupiga kura. Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kusafiri hupiga kura kati ya wake zake, kisha husafiri na yule aliyepata kura. Lililo wajibu ni kumuiga katika hilo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutokana na maneno Yake (´Azza wa Jall):
لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ
“Hakika mna kigezo kizuri kwa Mtume wa Allaah.”[1]
Jengine ni kwa sababu kusafiri kwake na mmoja wa wake zake bila maridhiano wala kupiga kura ni dhuluma kwa yule aliyeachwa au walioachwa. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ameharamisha dhuluma juu ya waja Wake na akaamrisha kufanya uadilifu.
[1] 33:21
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/237)
- Imechapishwa: 21/02/2026
Swali: Je, ni lazima kufanya uadilifu kati ya wake wawili baina yao katika safari?
Jibu: Ni wajibu awe mwadilifu baina yao katika safari kwa maridhiano au kwa kupiga kura. Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kusafiri hupiga kura kati ya wake zake, kisha husafiri na yule aliyepata kura. Lililo wajibu ni kumuiga katika hilo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutokana na maneno Yake (´Azza wa Jall):
لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ
“Hakika mna kigezo kizuri kwa Mtume wa Allaah.”[1]
Jengine ni kwa sababu kusafiri kwake na mmoja wa wake zake bila maridhiano wala kupiga kura ni dhuluma kwa yule aliyeachwa au walioachwa. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ameharamisha dhuluma juu ya waja Wake na akaamrisha kufanya uadilifu.
[1] 33:21
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/237)
Imechapishwa: 21/02/2026
https://firqatunnajia.com/uadilifu-kwa-aliye-na-mke-zaidi-ya-mmoja-katika-safari/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket