Swali: Je, imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba alikuwa akisoma katika swalah ya Fajr ”as-Sajdah” na ”al-Insaan”? Je, imesihi kutoka kwake kwamba alisujudu ndani ya swalah?

Jibu: Kinachotambulika kwa wanazuoni ni kwamba alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisujudu humo asubuhi ya ijumaa. Wala sijui makinzano yoyote ya wanazuoni katika hilo.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/264)
  • Imechapishwa: 20/02/2026