Mume amemlazimisha mkewe tendo la ndoa mchana wa Ramadhaan

Swali: Vipi kafara kwa mke ambaye amelazimishwa kufanya tendo la ndoa?

Jibu: Ikiwa amelazimishwa na hakuwa na khiyari kabisa, kwa maana alilazimishwa kufanya jambo hilo bila uwezo wa kukataa, basi hakuna kafara juu yake. Kafara itakuwa juu ya mume kwa nafsi yake mwenyewe.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (2/398)
  • Imechapishwa: 18/02/2026