Swali: Kukibaki kitu katika chakula kati ya meno ya mfungaji – Je, kitu hicho kinazingatiwa ni katika vifunguzi endapo atakimeza?

Jibu: Mfungaji akiamka na akakuta katika meno yake kuna mabaki ya chakula, kitu kama hicho hakiathiri funga yake. Lakini analazimika kutema na kuondosha mabaki haya. Katika hali hiyo haitoathiri swawm yake isipokuwa akikimeza. Akimeza kitu katika yale yaliyobaki kwenye meno yake kwa kukusudia, basi swawm yake inaharibika. Lakini akikimeza kwa ujinga au kwa kusahau hakuathiri swawm yake.

Muislamu anatakiwa kupupia kusafisha mdomo na meno yake baada ya chakula. Ni mamoja katika hali ya kufunga au nyenginezo. Kwa sababu usafi ni jambo linalotakikana kwa muislamu.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (02/401)
  • Imechapishwa: 18/02/2026