Swali: Baadhi ya watu wakati imamu anapokuwa katika swalah hali ya kurukuu huja kwa haraka, kisha mmoja wao huleta Takbiyr mbili; Takbiyr ya kufungulia swalah na Takbiyr ya kwenda katika Rukuu´; na baadhi yao huleta Takbiyr moja tu. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Kilichowekwa katika Shari´ah kwa maamuma anapokuja na imamu yuko katika Rukuu´ ni kutoharakisha. Bali atembee hali ya kuwa na utulivu na heshima, kisha aingie katika safu pamoja na imamu. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha kufanya hivo. Alete Takbiyr ya kufungulia swalah akiwa amesimama, kisha alete Takbiyr ya kwenda katika Rukuu´ wakati anainama kwenda Rukuu´. Ikiwa atatosheka na Takbiyr ya kuingia katika swalah tu, inamtosheleza ili aweze kuwahi Rak´ah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/151)
- Imechapishwa: 05/03/2026
Swali: Baadhi ya watu wakati imamu anapokuwa katika swalah hali ya kurukuu huja kwa haraka, kisha mmoja wao huleta Takbiyr mbili; Takbiyr ya kufungulia swalah na Takbiyr ya kwenda katika Rukuu´; na baadhi yao huleta Takbiyr moja tu. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Kilichowekwa katika Shari´ah kwa maamuma anapokuja na imamu yuko katika Rukuu´ ni kutoharakisha. Bali atembee hali ya kuwa na utulivu na heshima, kisha aingie katika safu pamoja na imamu. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha kufanya hivo. Alete Takbiyr ya kufungulia swalah akiwa amesimama, kisha alete Takbiyr ya kwenda katika Rukuu´ wakati anainama kwenda Rukuu´. Ikiwa atatosheka na Takbiyr ya kuingia katika swalah tu, inamtosheleza ili aweze kuwahi Rak´ah.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/151)
Imechapishwa: 05/03/2026
https://firqatunnajia.com/kuleta-takbiyr-moja-ili-kuwahi-rakah-nyuma-ya-imamu-kwenye-rukuu/