Swali: Imamu wa watu aliwakhutubia katika swalah ya ijumaa kisha akapatwa na maradhi wakati wa Khutbah ya mwisho ambapo akashuka baada ya kukamilisha Khutbah. Lakini hakuweza kusimama kwa sababu ya ukali wa maradhi yaliyompata. Kisha baada ya swalah kumalizika akazinduka kutokana na maradhi yale yaliyompata. Je, analipa swalah ya ijumaa au ya Dhuhr hali ya kuwa alizinduka ndani ya wakati na wakati haukupita au analipa Dhuhr?

Jibu: Mwenye kuwahi Rak´ah moja tu nyuma ya imamu katika swalah ya ijumaa basi huiswali Dhuhr. Hiyo ni kwa maana ya maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Yule mwenye kuwahi Rak´ah moja ya ijumaa basi ameiwahi swalah.”

Imepokewa na al-Athram.

Mtu huyu hakuingia pamoja na imamu katika swalah kabisa, hivyo huiswali Dhuhr.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/267)
  • Imechapishwa: 21/02/2026