Swali: Ni ipi hukumu ya kichinjwa kinachochinjwa kwa mnasaba wa kusalimika kutokamana na ajali?

Jibu: Ukifanya hivo kwa ajili ya kumshukuru Allaah ambapo ukawapa mafukara na ukawakusanya vilevile ndugu zako hakuna neno. Ukichinja kichinjwa kwa sababu ya kusalimika na ukawakusanya marafiki zako au kwa sababu ya kujenga nyumba mpya na ukawaalika ndugu na majirani  na ukawachinjia kwa ajili ya kumshukuru Allaah juu ya kile alichokuneemesha na mfano wa hayo, hakuna ubaya wowote. Kwa sababu kufanya hivo ni kwa ajili ya kumshukuru Allaah (Jalla wa ´Alaa). Sio katika Bid´ah.

Vivyo hivyo ikiwa mtu amefika kutoka safarini ambapo akawakusanya ndugu na akawachinjia [ni sawa]. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anapofika kutoka safarini anachinja kichinjwa fulani na anawakusanya wale ambao Allaah amempangia na wanakula.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/20990/%D9%85%D8%A7-%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%A7%D9%84%D8%B0%D8%A8%D8%A7%D9%89%D8%AD-%D9%84%D9%84%D9%86%D8%AC%D8%A7%D8%AD-%D8%A7%D9%88-%D8%A7%D9%84%D9%86%D8%AC%D8%A7%D8%A9-%D9%85%D9%86-%D8%AD%D8%A7%D8%AF%D8%AB
  • Imechapishwa: 04/01/2020