Swali: Je, kuna dalili ya baadhi ya walinganizi kutofautisha kati ya ´Aqiydah na mfumo wa kulingania kwa Allaah kwa njia ya kwamba ´Aqiydah yao ikawa ya Salafiyyah na mfumo wao katika kulingania ima ikawa ni wa ki-Ikhwaaniy au ki-Tabliyghiy?
Jibu: Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً
“Enyi mlioamini! Jisalimisheni kikamilifu.”[1]
Ni lazima kuufanyia kazi kwa pande zake zote. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):
فَلَمَّا زَاغُوا أَزَاغَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ
“Pindi walipopotoka, basi Allaah akazipotosha nyoyo zao.”[2]
Sisi si wenye kuleta vurugu katika dini hii. Ni lazima kuufanyia kazi Uislamu kwa pande zake zote bila kutenganisha kati ya misingi na matawi. Hiyo ni Bid´ah waliyozua, kama alivosema Haafidhw Ibn-ul-Qayyim katika kitabu chake “Swawaa´iq-ul-Mursalah”, yaliyozuliwa na al-Aswamm na Ibn ´Ulayyah; waliogawanya dini katika misingi na tanzu. Vinginevyo dini yetu yote ni misingi. ´Ibaadah zetu ni sehemu katika ´Aqiydah yetu na mambo yetu ya biashara ni sehemu katika ´Aqiydah yetu. Allaah hakuteremsha dalili yoyote juu ya mgawanyo huu. Baya zaidi kuliko haya ni kuigawanya dini katika maganda na nyama – mgawanyo huu ni Bid´ah ya kisasa.
Sisi tunamfuata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika ´Aqiydah na ulinganizi. Uongofu bora ni uongofu wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] 2:208
[2] 61:5
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 392-393
- Imechapishwa: 23/06/2025
Swali: Je, kuna dalili ya baadhi ya walinganizi kutofautisha kati ya ´Aqiydah na mfumo wa kulingania kwa Allaah kwa njia ya kwamba ´Aqiydah yao ikawa ya Salafiyyah na mfumo wao katika kulingania ima ikawa ni wa ki-Ikhwaaniy au ki-Tabliyghiy?
Jibu: Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً
“Enyi mlioamini! Jisalimisheni kikamilifu.”[1]
Ni lazima kuufanyia kazi kwa pande zake zote. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):
فَلَمَّا زَاغُوا أَزَاغَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ
“Pindi walipopotoka, basi Allaah akazipotosha nyoyo zao.”[2]
Sisi si wenye kuleta vurugu katika dini hii. Ni lazima kuufanyia kazi Uislamu kwa pande zake zote bila kutenganisha kati ya misingi na matawi. Hiyo ni Bid´ah waliyozua, kama alivosema Haafidhw Ibn-ul-Qayyim katika kitabu chake “Swawaa´iq-ul-Mursalah”, yaliyozuliwa na al-Aswamm na Ibn ´Ulayyah; waliogawanya dini katika misingi na tanzu. Vinginevyo dini yetu yote ni misingi. ´Ibaadah zetu ni sehemu katika ´Aqiydah yetu na mambo yetu ya biashara ni sehemu katika ´Aqiydah yetu. Allaah hakuteremsha dalili yoyote juu ya mgawanyo huu. Baya zaidi kuliko haya ni kuigawanya dini katika maganda na nyama – mgawanyo huu ni Bid´ah ya kisasa.
Sisi tunamfuata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika ´Aqiydah na ulinganizi. Uongofu bora ni uongofu wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] 2:208
[2] 61:5
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 392-393
Imechapishwa: 23/06/2025
https://firqatunnajia.com/kila-jambo-kwa-mujibu-wa-sunnah/