Kazi ya kuleta wafanyakazi nchi za warabuni

Swali: Baadhi ya watu wanawaleta wafanyakazi, kisha kuwaacha na kuchukua kutoka kwao kila mwezi kiasi maalum cha pesa.

Jibu: Mosi haijuzu kuwaleta makafiri, bali ni lazima kujihadhari kutokana na hilo. Ama waislamu, basi hakuna ubaya kuwaleta kwa njia iliyoruhusiwa na nchi. Nchi imeeleza namna ya uletaji. Kwa hiyo mwenye kuleta anatakiwa aende kwa mujibu wa yale ambayo dola imebainisha na kuyaweka. Hili ndilo wajibu kwa anayetarajia kuleta ili watu wasidhurike kwa kuletwa wale wasiofaa kuletwa.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30089/حكم-استقدام-العمال-واخذ-مبالغ-مالية-عليهم
  • Imechapishwa: 05/09/2025