Asili ya jibini zinazoletwa katika nchi za waislamu

Swali: Baadhi ya jibini huingizwa katika utengenezaji wake kitu kinachojulikana kama kimeng’enya cha ndama na jibini hizi ni za kuagizwa kutoka nje. Ni ipi hukumu yake?

Jibu: Asili katika jibini zinazopatikana miongoni mwa waislamu ni halali, mpaka ijulikane kuwa ndani yake kuna kitu najisi. Vinginevyo msingi wake ni uhalali. Vile vinavyoletwa kutoka nchi zetu, asili yake ni halali pia, isipokuwa ijulikane kwa hakika kuwa ndani yake kuna kitu kinachoharamisha.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (23/21)
  • Imechapishwa: 22/02/2026