Anayeswali ndani ya Hijr na Ka´bah iko nyuma yake

Swali: Ikiwa mtu ataingia ndani ya Hijr kisha akaifanya Ka´bah iwe nyuma yake – Je, swalah yake inasihi?

Jibu: Ndani ya Hijr yote imo katika Ka´bah isipokuwa upande mdogo tu, takriban dhiraa saba, zote ni katika Ka´bah. Hata hivyo inapaswa uso wake uwe umeelekezwa kwenye Ka´bah akiwa ndani ya Hijr, kwani Ka´bah ipo mbele yake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31614/ما-حكم-من-صلى-داخل-الحجر-والكعبة-خلفه
  • Imechapishwa: 08/11/2025