Allaah kuitia nguvu dini kupitia mtu muovu

Swali: Nini maana ya maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

”Hakika Allaah ataitia nguvu dini hii kwa mtu muovu.”?

Jibu: Ndani yake kuna dalili ya kwamba haki inaweza kutiwa nguvu kupitia mtu muovu kutokana na sababu kadhaa; ima kwa kujionyesha kwake, kuwanusuru watu wake, kunusuru nchi yake na sababu nyenginezo. Hakuikusudia dini. Pengine pia akaikusudia dini na kuitia nguvu dini, hata hivyo kwa lengo lingine lisilokuwa kumtakasia nia Allaah na kutafuta malipo kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Bali kutokana na sababu zingine. Kuna wapiganaji vita, wapigana jihaad na wenye kujionyesha ambao Allaah amenufaisha Uislamu kupitia wao ilihali sio katika watu wa kheri! Tukio hili ni ushahidi tosha juu ya hilo.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24391/معنى-ان-الله-ليويد-هذا-الدين-بالرجل-الفاجر
  • Imechapishwa: 05/10/2024