92. Je, ni katika hekima kuonyesha kutoridhika na kuwalalamikia watu wa kawaida?

Swali 92: Je, ni katika hekima kuonyesha kutoridhika na kuwalalamikia watu wa kawaida? Ni ipi njia sahihi ya kufanya hivo?

Jibu: Mambo hayo ni lazima yawe kwa mtawala au naibu wake. Kuonyesha kutoridhika na kuwalalamikia watu wa kawaida ni jambo linaenda kinyume na mfumo wa kisiasa ya Uislamu. Mwenendo kama huo unapelekea kukinzana na watawala. Haijuzu kwa yeyote kujiteua kuwa ni marejeo ya watu wote isipokuwa tu mtawala. Uasi juu ya watawala huanza namna hiyo:

وَمَن يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَىٰ وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّىٰ وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا

”Yeyote atakayempinga Mtume baada ya kuwa imeshambainikia uongofu na akaifuata njia isiyokuwa ya waumini, Tutamgeuza alikogeukia na tutamuingiza Motoni – na ni uovu ulioje mahali pa kuishia!”[1]

Hakuna vurugu katika Uislamu. Vurugu inakuwa katika mipangilio ya makafiri na wanafiki. Mpangilio wa Uislamu umepangwa na himdi zote njema ni stahiki ya Allaah.

[1] 4:115

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Ajwibah al-Mufiydah ´an As-ilat-il-Manaahij al-Jadiydah, uk. 223
  • Imechapishwa: 05/08/2024
  • taaliki: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy