Mushabbihah ni wale ambao wamezifananisha sifa za Allaah na sifa za viumbe.
Mu´tazilah ni wale ambao wamezikanusha sifa Allaah. Hoja yao eti wanamtakasa Allaah kutokana na mapungufu. Matokeo yake wakapetuka katika jambo hilo. Ni wafuasi wa Waaswil bin ´Atwaa´ na ´Amr bin ´Ubayd, wawili hao walikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wa al-Hasan al-Baswriy na walikuwa wakihudhuria katika duara zake za kielimu. Wakati al-Hasan al-Baswriy alipoulizwa kuhusu mtenda dhambi kubwa na akajibu kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah, kwamba Allaah ndiye atakayeamua cha kumfanya na hakufuru kwa dhambi hiyo kubwa ijapo imani yake ni dhaifu, hapo ndipo Waaswil alipomkemea na kumwambia kuwa yuko katika ngazi kati ya ngazi mbili – sio kafiri wala muislamu. Akazua ´Aqiydah hii batili. Matokeo yake akajitenga (اعتزل) na masomo ya al-Hasan. Wakakusanyika kwake watu ambao wana fikira moja kama yake, na wakaunda kikundi ambacho kikaitwa Mu´tazilah (المعتزلة).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 264-265
- Imechapishwa: 27/05/2025
Mushabbihah ni wale ambao wamezifananisha sifa za Allaah na sifa za viumbe.
Mu´tazilah ni wale ambao wamezikanusha sifa Allaah. Hoja yao eti wanamtakasa Allaah kutokana na mapungufu. Matokeo yake wakapetuka katika jambo hilo. Ni wafuasi wa Waaswil bin ´Atwaa´ na ´Amr bin ´Ubayd, wawili hao walikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wa al-Hasan al-Baswriy na walikuwa wakihudhuria katika duara zake za kielimu. Wakati al-Hasan al-Baswriy alipoulizwa kuhusu mtenda dhambi kubwa na akajibu kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah, kwamba Allaah ndiye atakayeamua cha kumfanya na hakufuru kwa dhambi hiyo kubwa ijapo imani yake ni dhaifu, hapo ndipo Waaswil alipomkemea na kumwambia kuwa yuko katika ngazi kati ya ngazi mbili – sio kafiri wala muislamu. Akazua ´Aqiydah hii batili. Matokeo yake akajitenga (اعتزل) na masomo ya al-Hasan. Wakakusanyika kwake watu ambao wana fikira moja kama yake, na wakaunda kikundi ambacho kikaitwa Mu´tazilah (المعتزلة).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 264-265
Imechapishwa: 27/05/2025
https://firqatunnajia.com/242-mushabbihah-na-mutazilah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
