1. Dibaji ya “Fusuwl fiys-Swiyaam wat-Taraawiyh waz-Zakaah”

Himdi zote njema anastahiki Allaah. Tunamhimidi Yeye, kumwomba msaada na msamaha na kutubia Kwake. Tunajilinda kwa Allaah kutokana na shari ya nafsi zetu na matendo yetu maovu. Yule mwenye kuongozwa na Allaah, basi hakuna wa kumpoteza, na yule anayepotezwa na Allaah, basi hakuna wa kumwongoza. Ninashuhudia ya kwamba hapana mungu mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allaah, hali ya kuwa peke yake hana mshirikina, na ninashuhudia kuwa Muhammad ni mja na Mtume Wake. Swalah na amani zimwendee yeye, jamaa zake, Maswahabah zake na yule mwenye kuwafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Ama baada ya hayo;

Kwa mnasaba wa kuja kwa mwezi wa Ramadhaan uliyobarikiwa ninawawasilishia ndugu zetu waislamu sura zifuatazo. Ninamuomba Allaah (Ta´ala) ajaalie kazi hii iwe imefanywa kwa ajili Yake pekee, iwe ni yenye kuafikiana na Shari´ah Yake na iwanufaishe waja Wake. Hakika Yeye ni mwingi wa kutoa na ni Mkarimu.

Sura ya kwanza: Hukumu ya swawm

Sura ya pili: Hekima ya swawm na faida zake

Sura ya tatu: Swawm ya mgonjwa na msafiri

Sura ya nne: Mambo yenye kuharibu swawm

Sura ya tano: Tarawiyh

Sura ya sita: Zakaah na faida zake

Sura ya saba: Wanaostahiki kupewa zakaah

Sura ya tisa: Zakaat-ul-Fitwr

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fusuwl fiys-Swiyaam wat-Taraawiyh waz-Zakaah, uk. 2
  • Imechapishwa: 03/06/2017