Swali: Kuna mwanamke ana deni la Ramadhaan. Anataka kulipa lakini mume wake amemuomba acheleweshe mpaka Sha´baan. Hata hivyo inajuzu kwake kulipa kabla ya hapo?

Jibu: Muda bado ukingali mpana. Ikiwa mume wake amemuomba kuchelewesha, acheleweshe. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa naye anatakiwa kulipa deni la Ramadhaan lakini anachelewesha mpaka Sha´baan kutokana na nafasi aliokuwa nayo kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kama ilivokuja katika Hadiyth.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy fiyl-´Aqiydah (11) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/msrf–09041434.mp3
  • Imechapishwa: 24/09/2020