Mtoto anataka kuacha kumtembelea mama yake anayemuona mkorofi

Swali: Kuna mtu anasema kwamba anapomtembelea mama yake au anapomfanyia wema, basi anakuwa na wivu mkubwa sana. Akimtembelea basi ni lazima kutazuka tatizo. Je, inafaa kwake kuacha kumtembelea ili kusizuke matatizo na asimwombee du´aa mbaya?

Ibn Baaz: Kwa nini anamuombea du´aa mbaya?

Mwanafunzi: Anaona wivu anapofanya jambo lolote kama vile kuzungumza na watoto wake au akizungumza na mke wake.

Jibu: Hapana, haijuzu kwake kumsusa mama yake. Anapaswa kuepuka jambo lolote linalomkasirisha. Anapaswa kumtembelea mama yake. Haya ni makosa, isipokuwa ikiwa atakasirika kwa jambo fulani, basi asizungumze maneno yatakayomkasirisha. Afanye kucheza na watoto au mke wake wakati mwingine. Si lazima acheze na mke au watoto wake mbele yake ilihali yeye mama hafurahishwi na jambo hilo. Atenge jambo hilo katika wakati mwingine.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25253/هل-يجوز-ان-يهجر-والدته-لشدة-غيرتها
  • Imechapishwa: 23/02/2025