Swali: Ni ipi hukumu ya kuweka kitu mdomoni kama vile karafuu wakati wa kuswali?

Jibu: Haijuzu kwa mwenye kuswali kuweka kitu mdomoni wakati wa kuswali. Kitu hicho kinamshughulisha kusoma au akahitaji kutafuna na kumeza, mambo ambayo yanapingana na swalah.

´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh

´Abdullaah bin Ghudayyaan

Swaalih al-Fawzaan

Bakr Abu Zayd

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (19811)
  • Imechapishwa: 13/05/2022