Inajuzu kwa mwanamke kuwaswalisha wanawake wenzake nyumbani kwa maiti?
Swali: Inajuzu kwa mwanamke kuwakusanya wanawake ambao ni ndugu wa maiti na akawaswalisha swalah ya jeneza kumswalia maiti wao ndani ya nyumba hiyo?
Jibu: Ndio. Ni sawa kwa mwanamke kuswali swalah ya jeneza. Ni mamoja akamswalia msikitini pamoja na wengine au akamswalia nyumbani kwa maiti huyo. Kwa kuwa wanawake hawakukatazwa kumswalia maiti. Walichokatazwa ni kuyatembelea makaburi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi, wale wenye kufanya ni mahali pa kuswalia na wale wenye kuyawekea mataa[1]. Hapa inahusiana na pale atapokusudia kuyatembelea. Upande mwingine ikiwa hakukusudia kuyatembelea, kwa mfano ameenda katika shughuli zake na akawa ameyapitia makaburi, ni sawa akasimama na akawatolea Salaam waliyomo ndani ya makaburi na akawaombea du´aa.
[1] Ahmad (01/229), Abu uDaawuud (3236), at-Tirmidhiy (320) aliyeifanya Hadiyth hiyo kuwa ni nzuri (Hasan), an-Nasaa´iy (2045).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/157-158)
- Imechapishwa: 15/09/2021
Inajuzu kwa mwanamke kuwaswalisha wanawake wenzake nyumbani kwa maiti?
Swali: Inajuzu kwa mwanamke kuwakusanya wanawake ambao ni ndugu wa maiti na akawaswalisha swalah ya jeneza kumswalia maiti wao ndani ya nyumba hiyo?
Jibu: Ndio. Ni sawa kwa mwanamke kuswali swalah ya jeneza. Ni mamoja akamswalia msikitini pamoja na wengine au akamswalia nyumbani kwa maiti huyo. Kwa kuwa wanawake hawakukatazwa kumswalia maiti. Walichokatazwa ni kuyatembelea makaburi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi, wale wenye kufanya ni mahali pa kuswalia na wale wenye kuyawekea mataa[1]. Hapa inahusiana na pale atapokusudia kuyatembelea. Upande mwingine ikiwa hakukusudia kuyatembelea, kwa mfano ameenda katika shughuli zake na akawa ameyapitia makaburi, ni sawa akasimama na akawatolea Salaam waliyomo ndani ya makaburi na akawaombea du´aa.
[1] Ahmad (01/229), Abu uDaawuud (3236), at-Tirmidhiy (320) aliyeifanya Hadiyth hiyo kuwa ni nzuri (Hasan), an-Nasaa´iy (2045).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/157-158)
Imechapishwa: 15/09/2021
https://firqatunnajia.com/inajuzu-kwa-mwanamke-kuwaswalisha-wanawake-wenzake-nyumbani-kwa-maiti/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)