Hukumu ya kuathiri ndoa kwa njia mbaya

Swali: Ni ipi hukumu kwa mtu ambaye anaathiri maisha ya ndoa ya mume na mke kwa njia mbaya? Mtu huyo ni katika jamaa wa karibu na mke.

Jibu: Ni haramu kumuharibia mwanamke kwa mume wake sawa bila kujali mwenye kufanya hivyo ni ndugu au sio ndugu. an-Nasaa´iy, Abu Daawuud na Ibn Hibbaan wamepokea kupitia kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kumuharibia mwanamke kwa mume wake sio katika sisi.”

Imepokewa na Abu Daawuud.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Fataawaa al-Qayyimah lil-Usrah al-Muslimah, uk. 47-48
  • Imechapishwa: 22/09/2020