Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
160 – Tunathibitisha Pepo juu ya wale kumi ambao walitajwa majina na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akawaahidi Pepo. Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni ya haki.
161 – Nao ni Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan, ´Aliy, Twalhah, az-Zubayr, Sa´d, Sa´iyd, ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf na Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah, ambaye ndiye mwaminifu wa Ummah huu. Allaah awawie radhi wote.
MAELEZO
Hawa kumi ndio ambao wamebashiriwa Pepo. Abu ´Ubaydah (Radhiya Allaah ´anh) amesifiwa kuwa ni mwaminifu wa ummah huu. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipoandika mkataba wa amani na Najraan na akawafaradhishia kulipa kodi, amesema Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh):
“Wakazi wa Najraan walikuja kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) wakasema: “Tutumie mtu mwaminifu, ee Mtume wa Allaah!” Akasema: “Nitakutumieni mtu mwaminifu kabisa.” Watu wakatazamia hilo. Akamwagiza Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah.”[1]
[1]al-Bukhaariy (3745) na Muslim (2420).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 234
- Imechapishwa: 27/04/2025
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
160 – Tunathibitisha Pepo juu ya wale kumi ambao walitajwa majina na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akawaahidi Pepo. Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni ya haki.
161 – Nao ni Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan, ´Aliy, Twalhah, az-Zubayr, Sa´d, Sa´iyd, ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf na Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah, ambaye ndiye mwaminifu wa Ummah huu. Allaah awawie radhi wote.
MAELEZO
Hawa kumi ndio ambao wamebashiriwa Pepo. Abu ´Ubaydah (Radhiya Allaah ´anh) amesifiwa kuwa ni mwaminifu wa ummah huu. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipoandika mkataba wa amani na Najraan na akawafaradhishia kulipa kodi, amesema Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh):
“Wakazi wa Najraan walikuja kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) wakasema: “Tutumie mtu mwaminifu, ee Mtume wa Allaah!” Akasema: “Nitakutumieni mtu mwaminifu kabisa.” Watu wakatazamia hilo. Akamwagiza Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah.”[1]
[1]al-Bukhaariy (3745) na Muslim (2420).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 234
Imechapishwa: 27/04/2025
https://firqatunnajia.com/215-watu-kumi-waliobashiriwa-pepo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
