Yesu akidhihirisha unyonge wake pindi walipotaka kumuua

39 Wakajibu: ”Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu40Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii. 41Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu:“Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.” 42Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma. 43Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho. 44Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.

  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Yohana 08:39
  • Imechapishwa: 16/01/2020